Subscribe:

Ads 468x60px

Wednesday, March 19, 2014

Rick Ross aamua kupunguza uzito wa mwili


Msanii Rick Ross kutoka pande za Marekani ameamua kuchukua maamuzi magumu ya kubadilisha aina ya maisha yake ili aweze kupunguza uzito mkubwa wa mwili alionao. Rick Ross ameamua kuchukua uamuzi huo uli kujiweka mbali na magonjwa mbalimbali yanayowakuta watu wenye uzito mkubwa kama presha.

Miaka miwili iliyopita Rick Ross alishawahi kuzimia ghafla akiwa katika ndege, hadi kusababisha ndege hiyo kutua kwa na msanii huyo akakimbizwa hospitali.  Baada ya kufanyiwa uchunguzi iligundulika kua uzito mkubwa alionao pamoja na kukosa usingizi ndio kilikua chanzo cha yeye kupoteza fahamu.

Baada ya hali hiyo ameamua kubadili mfumo mzima wa maisha yake ambapo anafanya mazoezi mara mbili kwa siku, huku akila chakula kwa ajili ya afya na kupata muda wa kupumzika.

0 comments: