Subscribe:

Ads 468x60px

Tuesday, March 11, 2014

Je Bayern Munich Watachezea Kichapo Nyumbani Kwao?

Ikiwa ni muendelezo wa michuano ya kuwania kombe la klabu bingwa barani Ulaya, kutakuwa na mechi mbili ambazo zitazichapa usiku wa leo. Arsenal, inaelekea, Bonn, kutoana jasho na mabingwa wa Ujerumani, Bayern Munich ambayo ilishinda mechi ya raundi ya kwanza kwa kichapo cha 2-0 katika uwanja wa Emirates.
Ikiwa ni mchezo wa marudiano, Arsenal itakosa huduma za mcheza kiungo wake Kieran Gibbs ambaye kwa sasa anauguza jeraha la mkuu na mshambulizi Yaya Sanogo, huku mlinda lango Laurent Koscielny ambaye alikuwa akiuguza jeraha la paja anatarajiwa kurejea.
                                  arsena
Kipa wa Arsenal Wojciech Szczesny, ambaye amesimamishwa kucheza kwa muda baada ya kupewa kadi nyekundu wakati wa mechi ya raundi ya kwanza,naye atachukuliwa nafasi na Lukasz Fabianski .
Ukiangalia kupitia historia ya timu ya Arsenal na Bayern kwa mwaka uliopita Arsenal iliishinda Bayern kwa magoli mawili kwa bila katika mechi ya marudiano lakini ilibanduliwa nje ya mashindano hayo baada ya kupoteza raundi ya kwanza 3-1.
Katika mechi nyingine ya marudiano leo usiku itakuwa kati ya Atletico Madrid Vs AC Milan. Madrid ilishinda awamu ya kwanza kwa bao moja kwa bila. Mario Balotelli huenda akajumuishwa kwenye kikosi cha wachezaji kumi na mmoja wa AC Millan, baada ya kuuguza jeraha la mgongo alilopata siku ya Jumamosi dhidi ya klabu ya Unidese.
Atletico nayo inamkaribisha mchezaji wake aliyefunga idadi kubwa ya magoli Diego Costa huku ikijaribu kufunzu kwa robo fainali ya kombe hilo kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka kumi na saba iliyopita.
Na ili kufuzu, mabingwa hao mara saba wa Ulaya ni sharti waandikishe historia ya kuwa timu ya tatu katika historia ya kombe hilo kuwahi kushindwa nyumbani katika mechi ya raundi ya kwanza na ishinde mechi ya marudiano ugenini.

0 comments: