Subscribe:

Ads 468x60px

Tuesday, March 18, 2014

Rapper Kanye West Apewa Adhabu Kali


Rapper Kanye West akiri mashitaka ya kumshambulia mpiga picha katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Los Angeles. Mpiga picha Paparazzi ,Daniel Ramos, alimtuhumu muimbaji huyo kwa kumpiga makonde na kumpokonya kamera yake. "nilikuwa nafanya kazi yangu wakati Kanye aliponishambulia, '' alisema mpiga picha huyo, '' ingekuwa ni mimi ningekuwa nimemfanyia kitendo hicho ningekuwa kizimbani.''

Mahakama imetoa Adhabu kwa muimbaji huyo mwenye umri wa miaka 36 kuwa  "ni kifungo cha nje cha miaka miwili na ameshurutishwa na mahakama kupata ushauri nasaha kuhusu anavyoweza kudhibiti hasira. Pia ametakiwa kuhudumia jamii kwa masaa 250 kwa kosa hilo alilofanya Julai mwaka jana".




Mpiga picha huyo anadai kuwa bado anatumia dawa kwa ajili ya majeraha aliyoyapa kutokana na kushambuliwa na West. Rapper Kanye alikamatwa mwaka 2008 kufuatia vurumai lengine na mpiga picha katika uwanja huohuo wa ndege. Kesi hiyo, ilitupiliwa mbali na mahakama baada ya West kuwalipia vifaa vilivyoharibika na pia kupata ushauri nasaha kuhusu namna ya kudhibiti hasira zake.

0 comments: