Subscribe:

Ads 468x60px

Featured Posts

Wednesday, March 19, 2014

Yanga na Azam Kuzichapa Leo

Klabu za Yanga na Azam FC leo zitakabiliana katika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mechi ya Ligi Kuu ya soka ya Tanzania Bara ambayo kimsingi itaweka wazi nafasi ya ubingwa kwa timu zote mbili baada ya dakika 90 kumalizika.
Yanga Sc ambao ni mabingwa watetezi wa soka la Tanzania Bara, wako pointi nne nyuma ya Azam FC inayoongoza kwa kuwa na pointi 43, lakini vijana wa Jangwani wakiwa wamecheza mechi moja pungufu. Azam imeshuka dimbani mara 19 wakati Yanga imeshuka mara 18.
Mbeya City ni wa tatu kwa kuwa na pointi 39 sawa na Yanga, lakini wakiwa na wastani mdogo wa mabao ya kufunga na kufungwa kulinganisha na kikosi cha Hans van de Pluijm.
Yanga imejichimbia Bagamoyo mkoani Pwani baada ya mechi yake ya mwishoni mwa wiki dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja
wa Jamhuri Morogoro ambako walitoka sare ya kutofungana.
Kwa upande wake, Azam FC inayonolewa na raia wa Cameroon, Joseph Omog, ilipata ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya
Coastal Union kwenye Uwanja wake wa Azam Complex, Chamazi.
Yanga inaingia uwanjani ikifahamu kuwa ilipoteza mechi ya kwanza dhidi ya Azam FC kwa mabao 3-2, hivyo si tu itataka kushinda ili kurejesha matumaini ya kutetea ubingwa wake, ila kulipiza kisasi.
Kocha wake, Pluijm amekaririwa akisema kuwa mechi ya leo ni kama fainali, kwani wakipoteza watakuwa wamepata pigo kubwa
katika kuelekea kwenye mbio za kurejesha taji Jangwani.

Rick Ross aamua kupunguza uzito wa mwili


Msanii Rick Ross kutoka pande za Marekani ameamua kuchukua maamuzi magumu ya kubadilisha aina ya maisha yake ili aweze kupunguza uzito mkubwa wa mwili alionao. Rick Ross ameamua kuchukua uamuzi huo uli kujiweka mbali na magonjwa mbalimbali yanayowakuta watu wenye uzito mkubwa kama presha.

Miaka miwili iliyopita Rick Ross alishawahi kuzimia ghafla akiwa katika ndege, hadi kusababisha ndege hiyo kutua kwa na msanii huyo akakimbizwa hospitali.  Baada ya kufanyiwa uchunguzi iligundulika kua uzito mkubwa alionao pamoja na kukosa usingizi ndio kilikua chanzo cha yeye kupoteza fahamu.

Baada ya hali hiyo ameamua kubadili mfumo mzima wa maisha yake ambapo anafanya mazoezi mara mbili kwa siku, huku akila chakula kwa ajili ya afya na kupata muda wa kupumzika.

Tuesday, March 18, 2014

Rapper Kanye West Apewa Adhabu Kali


Rapper Kanye West akiri mashitaka ya kumshambulia mpiga picha katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Los Angeles. Mpiga picha Paparazzi ,Daniel Ramos, alimtuhumu muimbaji huyo kwa kumpiga makonde na kumpokonya kamera yake. "nilikuwa nafanya kazi yangu wakati Kanye aliponishambulia, '' alisema mpiga picha huyo, '' ingekuwa ni mimi ningekuwa nimemfanyia kitendo hicho ningekuwa kizimbani.''

Mahakama imetoa Adhabu kwa muimbaji huyo mwenye umri wa miaka 36 kuwa  "ni kifungo cha nje cha miaka miwili na ameshurutishwa na mahakama kupata ushauri nasaha kuhusu anavyoweza kudhibiti hasira. Pia ametakiwa kuhudumia jamii kwa masaa 250 kwa kosa hilo alilofanya Julai mwaka jana".




Mpiga picha huyo anadai kuwa bado anatumia dawa kwa ajili ya majeraha aliyoyapa kutokana na kushambuliwa na West. Rapper Kanye alikamatwa mwaka 2008 kufuatia vurumai lengine na mpiga picha katika uwanja huohuo wa ndege. Kesi hiyo, ilitupiliwa mbali na mahakama baada ya West kuwalipia vifaa vilivyoharibika na pia kupata ushauri nasaha kuhusu namna ya kudhibiti hasira zake.

Mali Mpya Kutoka LIN COLLECTION

New arrivals at LIN COLLECTION....Handbags and Shoes..wahi mapema piece ni chache na za ukweli...piga 0767 898471 or Visit Facebook page www.facebook.com/LIN.Collection13



Friday, March 14, 2014

[Photo] Utengenezwaji wa Video Mpya ya Young Money

Tazama picha za kundi la Young Money likiongozwa na Lil Wayne,Nicki Minaj,Tyga, na wasanii wengine kibao,wakiwa kwenye utengenezwaji wa video ya wimbo mpya wa  Young Money "Tyga, Nicki Minaj & Lil Wayne" – Senile kutoka kwenye album yao mpya ya Rise Of The Empire.
111
81
19
26
55 (1)
73

Exclusive Kutoka LIN COLLECTION @Sinza.

Kwa wale wajanja wa Town, Jipatie Handbags,Sandals,Shoes kaliii toka (Thailand,Italy,Northern Europe), Tembelea LIN COLLECTION iliyopo Sinza Makaburini Bus Station... Kujipatia na Mzigo mkalii.. usikose kutembelea duka hilo ili kujipatia vitu special. Kwa mawasiliano zaidi; 0767 898471














Van Persie Atasaini Mkataba Mpya Man Utd..?

Mshambuliaji wa Manchester UnitedRobin van Persie amesema kuwa yuko tayari kuongeza muda wa mkataba wake.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30, amekuwa akihusishwa na madai ya kutaka kukihama klabu hiyo kwa kuwa hana uhusiano mwema na kocha wa David Moyes na kumekuwa na fununu kuwa huenda akaondoka mwishoni mwa wa msimu huu. Lakini mchezaji huyo kutoka Uholanzi amesema kuwa anaridhika kucheza chini ya Moyes.